Makamu Mkuu Wa Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo Prof Raphael Chibunda Awataka Watumishi Wa Kampasi Ya Mizengo Pinda Kufanya Kazi Kwa Ushirikiano

Prof. Chibunda amewataka watumishi wa Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda kufanyakazi kwa ushirikiano ili kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kampasi hiyo. Aliyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi ya siku mbili katika Kampasi ya Mizengo Pinda Novemba 7 – 8, 2022.

Katika ziara hiyo, Prof. Chibunda alipokea ripoti ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Kampasi hiyo na kupata fursa ya kutembelea miradi hiyo.

Pia, Prof. Chibunda aliongeza kusema kwamba kupitia serikali ya awamu ya sita imedhamiria kuboresha sekta ya elimu ya juu nchini ikiwemo Kampasi ya Mizengo Pinda.  Kiasi cha pesa takribani bilioni ishirini zimetengwa kwa ajili ya kuboresha na kuendeleza Kampasi ya Mizengo Pinda. Pesa hizo zinatarajiwa kutumika kujenga majengo matatu ambayo ni jengo la Taaluma linalokadiriwa kuchukua wanafunzi zaidi ya elfu mbili (2000) kwa wakati mmoja, maabara za kufundishia pamoja na dahalia.

Related Posts

SUA-MPC Students Gain Practical Agricultural Experience Through Empien Company Limited Collaboration

Students from the Mizengo Pinda Campus (MPC) of Sokoine University of Agriculture (SUA) have gained invaluable hands-on experience in seed...

SUA-Mizengo Pinda Campus Leadership Visits Mpimbwe Radio to Discuss Achievements and Opportunities

The Acting Principal of the Sokoine University of Agriculture—Mizengo Pinda Campus, Professor Anna Sikira, along with the Acting Head of...

SUA Students Benefit from Practical Training in Tour Guiding and Environmental Conservation

The Sokoine University of Agriculture (SUA) – Mizengo Pinda Campus, in collaboration with Nomad Safari and the Watu, Simba na...