Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Atembelea Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo Kampasi ya Mizengo Pinda

Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Techknolojia, Mh. Omary Juma Kipanga akiteta jambo na mwenyeji wake Rasi wa Ndaki ya Mizengo Pinda, Prof Josiah Katani na mkuu wa wilaya ya  Mlele Mh Sanga pindi alipotembelea katika kampasi hiyo.

Wakati huohuo Mh. Kipanga alipata nafasi ya kuzungumza na watumishi wa SUA, Viongozi wa halmashauri ya Mlele pamoja na wajumbe wa kamati ya siasa ya wilaya.

Mh. Kipanga amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mh Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kuboresha sekta ya Elimu na katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Sua Kampasi ya Mizengo Pinda imetengewa kiasi cha shilingi Billioni ishirini kwaajili ya ujenzi wa majengo matatu, Jengo la Taaluma, Jengo la Mabweni na Jengo la Daharia.

Pia, Mh. Kipanga amemtaka Rasi wa Ndaki Prof. Josiah Katani kusimamia vyema  fedha inayotolewa na Mh. Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania iendane na thamani ya majengo yatakayojengwa kwa maendeleo ya sekta ya Elimu na Nchi kiujumla.

Related Posts

SUA-MPC Students Gain Practical Agricultural Experience Through Empien Company Limited Collaboration

Students from the Mizengo Pinda Campus (MPC) of Sokoine University of Agriculture (SUA) have gained invaluable hands-on experience in seed...

SUA-Mizengo Pinda Campus Leadership Visits Mpimbwe Radio to Discuss Achievements and Opportunities

The Acting Principal of the Sokoine University of Agriculture—Mizengo Pinda Campus, Professor Anna Sikira, along with the Acting Head of...

SUA Students Benefit from Practical Training in Tour Guiding and Environmental Conservation

The Sokoine University of Agriculture (SUA) – Mizengo Pinda Campus, in collaboration with Nomad Safari and the Watu, Simba na...