Safari ya Mhitimu wa SUA Kuelekea Ujasiriamali wa Bidhaa Zitokanazo na Rasilimali  Nyuki

Katika picha, aliyeshika chupa za asali ni Dwasi Denis Johnson, mhitimu wa Shahada ya Sayansi ya Awali ya Usimamizi wa Rasilimali Nyuki. Anatumia ujasiriamali wa bidhaa zitokanazo na rasilimali nyuki, kama asali ya nyuki wakubwa na wadogo, katika maonesho ya Wiki ya Mwanakatavi ambayo hufanyika kila mwaka mkoani Katavi. Maonesho haya yana lengo la kuwakutanisha wajasiriamali, taasisi, wakulima, wafugaji na kutangaza utalii na fursa zote zipatikanazo katika mkoa wa Katavi.

Bw. Dwasi amemshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpimbwe, Bi. Shamimu Mwariko, kwa kuendelea kuwapa ushirikiano kama wajasiriamali wa Halmashauri ya Mpimbwe.

Kwa sasa, Bw. Dwasi ana mizinga ishirini (20) iliyopo kwenye kijiji cha Kanindi, yenye uwezo wa kutoa lita 15 hadi 20 za asali. Hivyo, Bw. Dwasi anawaomba wadau ambao wanaweza kumsaidia kupata mizinga ya kisasa inayogharimu kiasi cha shilingi milioni mbili (2,000,000) ili aweze kuzalisha zaidi asali.

Katika picha: Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Rungwa wakipata elimu kuhusu uzalishaji wa asali kupitia mdudu nyuki na kalenda sahihi ya uandaaji wa mizinga. Elimu hii ilitolewa walipotembelea banda la Halmashauri ya Mpimbwe katika Maonesho ya Wiki ya Mwanakatavi.

Related Posts

SUA-MPC Students Gain Practical Agricultural Experience Through Empien Company Limited Collaboration

Students from the Mizengo Pinda Campus (MPC) of Sokoine University of Agriculture (SUA) have gained invaluable hands-on experience in seed...

SUA-Mizengo Pinda Campus Leadership Visits Mpimbwe Radio to Discuss Achievements and Opportunities

The Acting Principal of the Sokoine University of Agriculture—Mizengo Pinda Campus, Professor Anna Sikira, along with the Acting Head of...

SUA Students Benefit from Practical Training in Tour Guiding and Environmental Conservation

The Sokoine University of Agriculture (SUA) – Mizengo Pinda Campus, in collaboration with Nomad Safari and the Watu, Simba na...